Mwanzo » » DOGO JANJA TANGU KUAZA MUZIKI WAKE MPAKA SASA ANACOLLOBO MOJA TU LA KUSHIRIKISHWA.

DOGO JANJA TANGU KUAZA MUZIKI WAKE MPAKA SASA ANACOLLOBO MOJA TU LA KUSHIRIKISHWA.

Imewekwa ma Unknown siku Wednesday 16 October 2013 | 08:10

ALIKUWA DOGO JANJA NA SASA NI JANJARO

Kwa kawaida msanii anapotoka na kuhit sana huombwa kushirikishwa kwenye nyimbo za wasanii wenzake nyingi na tumekuwa tukiona baadhi ya wasanii wakidiriki kusema wamesitisha kufanya collabo na wasanii ama wanahitaji kulipwa kiasi flani cha pesa na anaetaka kuwashirikisha.
Hii ni tofauti kwa mkali wa michano yenye style yenye ladha ya Kaskazini Janjaro, ambae pamoja na kuwa na hits nyingi hewani na kupiga show hadi Afrika Kusini, ameshawahi kushirikishwa kwenye wimbo mmoja tu tangu aanze muziki, I mean tangu akiwa Arusha wakati hajaingia kwenye mkondo mkubwa wa Muziki TZ (Main stream).
“Nilishawahi kushirikishwa kwenye wimbo mmoja tu unaoitwa ‘Shikamoo Mwalimu’, nilifanya na Easy Muchwa, ma-producer walioufanya ni P-Funk Majani na Chizan Brain, ile ya Madee (Nisikilize) nilifanya intro tu na sikuandikwa kama nimeshirikishwa. Nilipokuwa Arusha nilifanya nyimbo zangu tu lakini sikushirikishwa.” Janjaro ameiambia tovuti ya Times Fm.
Wimbo aliofanya na Asley(Nimeshamaliza) ulikuwa wimbo wao wa pamoja. Janjaro ameshawashirikisha wasanii kadhaa kwenye project zake akiwemo Tunda Man, Chege, Godzilla, PNC, Jambo Squared na wengine.
Hata hivyo Janjaro atakuwa kwenye Project kubwa ya Dj Choka itakayowashirikisha wasanii wenye umri mdogo, na waliotajwa kushiriki ni pamoja na Young Dee, Country Boy na M-Rap. Project hiyo inafanyika katika studio za BHitz chini ya producer Pancho.

Huu ndio wimbo pekee aliowahi kushirikishwa officially Janjaro:

CHANZO: TIMES FM SITE.
Share habari hii :

Post a Comment

WADHAMINI WA BLOG YETU

SIKILIZA CLOUDS FM ONLINE HAPA

TUFUATE HAPA

WASOMAJI WETU

FACEBOOK

DONDOO ZA MWEZI

TWITTER

BLOG ZA WADAU

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
HAKIMILIKI © 2013. CLICK BONGO TZ - Haki zote zimehifadhiwa