Mwanzo » » AFANDE SELE ATAFUTA PESA KUPITIA BONGO MOVIE NA ''FILAMU YANGU''

AFANDE SELE ATAFUTA PESA KUPITIA BONGO MOVIE NA ''FILAMU YANGU''

Imewekwa ma Unknown siku Sunday 1 December 2013 | 11:05

SELEMEN MSINDI ''AFANDE SELE''
MFALME wa mistari, Selemani Msindi ‘Afande Sele,’ amesema yuko mbioni kuachia filamu yake mpya itakayofahamika kwa jina la ‘Filamu Yangu.’
Akizungumza jana na Tanzania Daima, Afande Sele alisema kuwa filamu hiyo itazungumzia maisha halisi ya Kitanzania.
Alisema ameamua kujikita katika uigizaji wa filamu kutokana na filamu nyingi za sasa kutokuwa na maadili halisi ya Kitanzania, hivyo anataka kuonyesha njia.
“Mimi nikiangalia filamu za hao wanaojiita ma-superstar, sifiki mwisho na sijawahi kuangalia filamu yoyote ya kibongo hadi mwisho, zinaboa na unaona hakuna uhalisia wa jambo husika, watu wanaiga Wanigeria mwanzo-mwisho, wanakera,” alisema.
Afande Sele alisema kuwa ujio wa ‘Filamu Yangu’ utakuwa wa tofauti kuanzia picha, maadili na namna wasanii wake watakavyoigiza.
Aliwataka Watanzania kukaa mkao wa kula kwani filamu hiyo ipo jikoni ikipikwa kwa ustadi mkubwa.
Share habari hii :

Post a Comment

WADHAMINI WA BLOG YETU

SIKILIZA CLOUDS FM ONLINE HAPA

TUFUATE HAPA

WASOMAJI WETU

FACEBOOK

DONDOO ZA MWEZI

TWITTER

BLOG ZA WADAU

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
HAKIMILIKI © 2013. CLICK BONGO TZ - Haki zote zimehifadhiwa