Kesi inayomkabili Msanii wa miondoko ya mduara anayefanya vyema sana, kesi yake na mganga wa tiba za asili imehairishwa hadi tarehe 24 april baada ya AT kuchelewa kufika mahakamani
Kesi hiyo ambayo ilifunguliwa na Mganga wa kienyeji Sharif katika mahakama ya mwanzo Buguruni kwa mara ya kwanza tarehe 10 mwezi march akiwa anamdai AT fedha baada ya kutumia huduma za mganga huyo bila kulipa na AT alikanusha madai hayo na Hakimua kaamua kuipiga kalenda kesi hiyo hadi tarehe ya leo.
AT alifika Mahakamani akiwa amechelewa na akatoa sababu za msingi kwa nini amechelewa na Hakimu wa Kesi hiyo akamwelewa na kuamua kuiairisha lakini pia AT alisema mganga huyo kama kweli ana mdai aje na ushaidi wake kama vile mkataba wa risiti kama alitumia huduma hizo.
Post a Comment