Mwanzo » » DK. CHENI AZUNGUMZA KUHUSU TAARIFA ZA YEYE KUWA FREEMASON.

DK. CHENI AZUNGUMZA KUHUSU TAARIFA ZA YEYE KUWA FREEMASON.

Imewekwa ma Unknown siku Wednesday 26 February 2014 | 20:48

Zimekuwepo taarifa za kuwa Dk. Cheni muigizaji wa filamu za Kibongo na Mc wa shughuli mbali mbali amekuwa akizushiwa kuwa yeye ni miongoni mwa members wa Freemason kutoka Tanzania na baadhi ya mambo yanayotwa kuonesha kuwa Dk. Cheni ni Freemason ni pamoja na mafanikio yake kuwa makubwa ingawa katika uwezo wa kufanya sanaa uko chini ukilinganisha na wasanii wenzake anaofanya nao sanaa.


Lakusikitisha zaidi ni kuwa hata watu wake wa karibu wanamnyooshea vidole Dk Cheni wakimuitwa Freemason na majina ya wanaomsema kwa hilo tumeyaifadhi na zaidi mmoja wapo kati ya walioweza kuzungumza na mwanahabari wetu alidai kuwa

''kila dalili inaonyesha Dk. Cheni ni freemason, angalia mavazi yake mengi ni meusi, machata na alama kibao zinazohusishwa na taasisi hiyo, angalia fedha aliyonayo, angalia hata gari lake lilivyojaa alama za ajabu ajabu, huyu jamaa ni Freemason kabisa'' Alisema mmoja ya wadau walio zungumza na kwa usalama wale hakutaka jina lake litajwe nasi tunalihifadhi.

Katika kutaka kuupata ukweli wa fununu hizi ilibidi atafutwe Dk. Cheni na hapa chini alifunguka kama ifuatavyo...
''Dah! na wewe umeyapata kaka,hakika naumia sana na madai hayo, yamevuma sana kwa wadau, tena baadhi yao ni watu ninaowaheshimu sana, jamani mimi sio Freemason, naigiza kazi zangu za u-mc zinaniingizia kipato, najiwekea akiba''.

Si mtu wa starehe, nawekeza katika biashara ndogo ndogo, madai haya ya Freemason yananitesa sana ila namuachia mungu'' Dk. Cheni aliongeza kusema



Share habari hii :

Post a Comment

WADHAMINI WA BLOG YETU

SIKILIZA CLOUDS FM ONLINE HAPA

TUFUATE HAPA

WASOMAJI WETU

FACEBOOK

DONDOO ZA MWEZI

TWITTER

BLOG ZA WADAU

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
HAKIMILIKI © 2013. CLICK BONGO TZ - Haki zote zimehifadhiwa