Stori: Shani Ramadhani
Msanii wa filamu, Deogratias Shija ‘Shija’ ameeleza kuwa, mpaka sana angekuwa ameshafunga ndoa ila kinachokwamisha mambo ni mchumba wake anayemalizia masomo.
Msanii wa filamu, Deogratias Shija ‘Shija’ ameeleza kuwa, mpaka sana angekuwa ameshafunga ndoa ila kinachokwamisha mambo ni mchumba wake anayemalizia masomo.
Akipiga stori na Ijumaa juzikati, Shija alisema anajua baadhi ya mashabiki na marafiki zake wanashangaa kuona kimya kuhusiana na suala la yeye kufunga ndoa ila akasema, wavute subira kwani mchumba wake huyo akimaliza tu masomo, ndoa itafungwa.
“Kinachonichelewesha kufunga ndoa ni kwamba namsubiri mchumba wangu amalize kwanza masomo yake ya chuo ndipo mipango iendelee kwani anabanwa sana, nataka nikimuoa awe amemaliza chuo,” alisema Shija bila kutaja jina la mchumba wake na chuo anachosoma.
Post a Comment