Mwanzo » » CHECK ORODHA YA MATAJIRI 5 KATI YA MATAJIRI WAKUBWA 40 AFRIKA.

CHECK ORODHA YA MATAJIRI 5 KATI YA MATAJIRI WAKUBWA 40 AFRIKA.

Imewekwa ma Unknown siku Monday 31 March 2014 | 16:56

SAID SALIM BACKHRESA ANAANZA KISHA Gulam Dewji anafuatia akishika nafasi ya pili huku Rostam Aziz akishika nafasi ya 3,Reginald Mengi anashika nafasi ya 4 na wa tano ni Ali Mufuruki.


1.SAID SALIM BACKHRESA .

Anamiliki mali na fedha zenye thamani ya Dola za Marekani 620 Million sawa na Tsh.992 Bilion(Dola 1=1600)
Utajili wake unatokana na mapato yanayotokana na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali kwenye viweanda vyake.
Inasemekana kua Bakhresa aliacha shule akiwa na miaka 14 miaka ya 1970 na kuanzisha shughuli zake za biashara ndogondogo za uuzaji wa Urojo Huko Zanzibar.
Baada ya mda alifungua Mgahawa,akanzisha mashine ya kusaga nafaka kisha akaanzisha viwanda vya usindikizaji wa vyakula kama vile mikate,kutengeneza chokolate,Icecream na vinywaji Baridi. 

2 ALHAJ MOHAMED.GULAM DEWJI.


Ana mali na fedha zenye thamani ya Dola 560 Milion. 
Ni sawa na Bilion 896 za Kitanzania.
Utajiri wa Dewji unatokana na kuzalisha bidhaa na kutoa huduma mbalimbali.
Anamiliki makampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania inayofanya kazi Afrika Mashariki na Kati,21st century Textile,Kampuni ya Bima,Makampuni ya kuuza mafuta ya Petrol na maduka mbalimbali zaidi ya 100 Tanzania.




3.ROSTAM AZIZ

Ana mali na fedha zenye thamani ya Dola 420Milion sawa na Tsh.672 Bilion.
Utajiri wake unatokana na kumiliki Hisa za makampuni ya mawasiliano ya simu,madini,Biashara za Usafiri wa Meli.
Anamiliki asilimia 19 ya Hisa za Kampuni ya Vodacom.
Amewahi kua mbunge wa Igunga kwa kupitia CCM Kuanzia mwaka 1995-2011.


4.REGINALD MENGI.
Ana mali na Pesa zenye thamani ya Dola 280 Milion. 
Sawa na Sh.448 Bilion.


Anamiliki Kampuni mbalimbali Ikiwemo vyombo mbalimbali(Ni Mkurugenzi wa Makampuni ya IPP- Medi,yenye vyombo vya Habari vya ITV,RADIO ONE,EATV,EATV RADIO,CAPITAL RADIO,CAPITAL TELEVISION).
Anamiliki viwanda vinavyozalisha vinywaji Baridi vya Coca cola na Mgodi wa Dhahabu.

5. ALI  MUFURUKI.
Anamiliki mali na Pesa zenye thamani ya Dola 110 Milion(176 Bilion)
Utajiri unatokana na kazi ya Uendelezaji Makazi na Ukodishaji,Matangazo na Shughuli za mawasiliano.
Ni mkurugenzi wa Info Tech Investment LTD-Dar Es Salaam.
Ni mwenyekiti wa Mwanachi Communications LTD(yenye magazeti ya Mwananchi na The Citizen)
 NB:Wamepatikana kutokana na nafasi zao kifedha,ufanisi wa kampuni zao ktk soko la hisa,mfumo wa wanahisa ktk soko la hisa,na mtiririko mzima wab kifedha ktk kaunti zao kwenye benki mbalimbali.


Share habari hii :

Post a Comment

WADHAMINI WA BLOG YETU

SIKILIZA CLOUDS FM ONLINE HAPA

TUFUATE HAPA

WASOMAJI WETU

FACEBOOK

DONDOO ZA MWEZI

TWITTER

BLOG ZA WADAU

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
HAKIMILIKI © 2013. CLICK BONGO TZ - Haki zote zimehifadhiwa