Mwanzo » » YANGA SC Vs. AL AHLY KIMENUKA UWANJA WA TAIFA FUJO YATANDA.

YANGA SC Vs. AL AHLY KIMENUKA UWANJA WA TAIFA FUJO YATANDA.

Imewekwa ma Unknown siku Saturday 1 March 2014 | 17:05

clip_image002


Katika hali isiyokuwa ya kawaida,Mashabiki wa timu ya Simba wameanza tena kung'oa viti vya kukalia uwanjani hapa na kuwatupia Mashabini wenzao wa Timu ya Yanga waliofurika kwa wingi uwanjani hapa,kwa kile kinachodaiwa kuwa hawataki kukaa nao sehemu moja.lakini kwa hali ilivyo hivi sasa Uwanjani hapa,ni dhahiri kabisa kuwa Mashabiki hao wa Yanga wanaweza kuujaza Uwanja huu hasa kwa jinsi wanavyozidi kuingia Uwanjani hapa.Uongozi wa Vilabu hivi viwili vikubwa hapa nchini unatakiwa kukaa chini na Mashabiki wao na kuwakanya kuhusiana na uharibifu wa Miundombinu wanaoufanya Mashabiki wao katika Uwanja huu wa Taifa,kwani kuendelea kwa vitendo hivi kunazorotesha sana soka letu.Picha zote na Othman Michuzi,Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Ma
shabiki wa Timu ya Simba wakiendelea kuwarushia viti Mashabiki wa timu ya Yanga kabla hata ya mtanange wenyewe kuanza uwanjani hapa.Viongozi wa timu ya Yanga wakiwaomba Mashabiki wao kuhama katika eneo hilo na kwenda kujibana katika eneo walilotengewa kama wana Yanga.Mashabiki wa timu ya National Al Ahly wakiongea na Askari Polisi kuomba wakalizuie tatizo hilo.Askari Polisi wakiongea na Viongozi wa Timu ya Yanga ili waweze kwenda kuwaomba mashabiki wao waaondoke katika upande ule unaodaiwa kuwa ni wa Mashabiki wa Simba.Mambo yalianza kama masihara huku wengine wakitaniana kabisa.Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya wenyeji Young Africans Vs Al AhlyKIKOSI CHA NACIONAL AL AHLY Ekramy, Moawad, Nagiub, Wael Gomaa, Fathy, Rabea, Ashaur, Mousa Edan, Gedo, na Amri GamalKIKOSI CHA YANGA KINACHOANZA LEOclip_image0031. Deogratias Munish "Dida" - 302. Mbuyu Twite - 63. Oscar Joshua - 44. Nadir Haroub "Cannavaro" - 23 (C)5. Kelvin Yondani "Cotton" - 66. Frank Domayo "Chumvi" - 187. Saimon Msuva - 278. Haruna Niyonzima - 89. Emmanuel Okwi - 2510. Mrisho Ngasa - 1711. Hamisi Kizza - 20Subs:1. Juma Kaseja - 12. Juma Abdul - 123. David Luhende - 34. Athuman idd "Chuji" - 245. Hassan Dilunga - 266. Said Bahanuzi - 117. Didier Kavumbagu – 7KICK OFF1' Young Africans 0 - 0 Al Ahly3' Al Ahly wanalishambulia lango la Yanga lakini Dida anaokoa hatari5' Yanga wanapata kona na inaokolewa na Al Ahly07’ Yanga wametawala kati, Msuva na Niyonzima wanaonana vizuri. (0-0)09’ Msuva anacheza fyongo pale. (0-0)10’ Penaltyyyyyy hapana Refa anakataa kwa madai mshambuliaji wa Al Ahly alijidondosha. (0-0)11’ Yanga wanapata kona ya pili inaokolewa na wachezaji wa Ahly. (0-0)14' Yanga 0 - 0 Al AhlyDakika ya 15, Young Africans 0 - 0 Al AhlyDakika 20.. .Shuti kali la umbali lililopigwa na Frank Domayo nusu litinge wavuni sharif Ahmad akaudokoa na kuutoa nje ikawa konaDakika 22.okwiiiiiiiiii. . Nusura aipatie yanga goli. . Na kipa wa Al ahly anaanguka na kudai kaumia. .Yanga 0 Al Ahly 0
DAKIKA YA 30 Mchezaji wa  AL AHLY anapata kadi ya Manjano baada ya kumchezea vibaya Emanuel Okwi
DAKIKA YA 37 Yanga wanaonekana kushambulia sana Goli la AL ahly lakini wanakosa umakini na kufanya kusa nafasi nyingi za magoli ya wazi hapa
DAKIKA YA 40. .Yanga wanashambulia kwa kasi lango la Al Ahly na kupata kona takribani 3 na kukosa magoli kupitia kwa Hamis kiiza na Emanuel Okwi. . AL AHLY wanacheza taratibu na kupoza mpira huku wakijaribu mashambulizi ya kushtukizaDAKIKA 3 ZA NYINGEZA BAADA YA DAKIKA 45 KUMALIZIKA
Yanga Wanakosa Kona nyingine tena hapa
Share habari hii :

Post a Comment

WADHAMINI WA BLOG YETU

SIKILIZA CLOUDS FM ONLINE HAPA

TUFUATE HAPA

WASOMAJI WETU

FACEBOOK

DONDOO ZA MWEZI

TWITTER

BLOG ZA WADAU

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
HAKIMILIKI © 2013. CLICK BONGO TZ - Haki zote zimehifadhiwa